Sunday, November 25, 2012

RAISI WA UTPC NDANI YA KIGOMA PRESS




Raisi wa Muungano wa vilabu vya waandishi wa habari nchini (UTPC) Keneth Simbaya (wa pili kulia) akimsindikiza Mkuu wa wilaya kigoma (wa pili Kushoto) baada ya kufungua mkutano wa wadau na kuzindua blog ya Kigoma Press Club (kushoto) ni Mwenyekiti wa KGPC Deo Nsokolo na kulia ni Katibu Tawala wa wilaya Kigoma


Raisi wa Muungano wa vilabu vya waandishi wa habari nchini Keneth Simbaya Kati kati akiwa katika ofisi za Kigoma Press Club muda mfupi baada ya kuwasili mkoani humo kuhudhuria mkutano wa wadau wa habari na mkutano mkuu maalum wa Kigoma Press Club (kushoto) ni Mwenyekiti Deo Nsokolo na (kulia) ni Mwanachama Winfrida Bwire.

Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Kigoma Deo Nsokolo (wa pili kushoto) akimueleza jambo Mkuu wa wilaya Kigoma (katikati) kuhusu blog ya chama cha waandishi wa habari mkoa Kigoma wakati wa mkutano wa wadau (wa pili kulia) ni Raisi wa muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania Keneth Simbaya (Picha na Fadhili Abdalla)

WADAU KUTOKA TAASISI NA MASHIRIKA MBALIMBALI MKOANI KIGOMA WAKISHUHUDIA UZINDUZI WA BLOG YA KIGOMA PRESS CLUB

BAADA YA UZINDUZI MKUU WA WILAYA KIGOMA RAMADHANI MANENO ALIYOA NENO KWA WADAU NA WAANDISHI WA HABARI WALIOHUDHURIA MKUTANO WA WADAU MKOANI KIGOMA

Thursday, November 22, 2012

MSAADA KUTOKA WORLD LUNG FOUNDATION

 mkuu wa mkoa Kigoma Issa Machibya akipokea msaada wa moja ya mashine tano za upasuajia zenye thamani ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya vituo vitano vya afya mkoani Kigoma kutoka kwa Brigita Steffan (Katikati) Mke wa mkurugenzi wa miradi wa shirika la World Lung Foundation Staffan Bergstrom (kulia) katika hafla ya kukabidhi mashine hiyo kwa ajili ya Kituo cha Afya Ujiji Manispaa ya Kigoma Ujiji



Mkuu wa mkoa kigoma Issa Machibya akikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa huduma za upasuaji katika kituo ch afya Ujiji manispaa ya Kigoma Ujiji kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la World Lung Foundation Steffan Bergstrom.

SHIRIKA la Wolrd Lung Foundation lenye makao yake makuu nchini Marekani
limetoa msaada wa vifaa vya upasuaji kwa ajili ya  kituo cha afya cha Ujiji
manispaa ya Kigoma Ujiji ili kusiadia upasuaji kwa kina mama wajawazito
wanaoapata matatizo wakati wa kujifungua.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 100 vilikabidhiwa kwa Mkuu
wa mkoa Kigoma,Issa Machibya na Brigita Staffan mke wa Mkurugenzi wa miradi
wa shirika hilo hapa nchini, Staffan Bergstrom.

Akikabidhi wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo Mkurugenzi wa miradi wa
World Lung Founation nchini, Staffan Bergstrom alisema kuwa ni wazi kuanza
kutumika kwa vifaa hivyo itakuwa mkombozi mkubwa kwa kina mama ambao upata
matatizo wakati wa kujifungua na wakati mwingine kufa.

Alisema kuwa shirika hilo limetoa mchango huo ikiwemo ni sehemu ya pato la
Meya wa Jiji la London, Peter Bloomber ambaye aliamua kujitolea sehemu ya
pato lake kwa ajili kusaidia matibabu ya kina wanaopata matatizo wakati wa
kujifungua.
 

Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa mkoa kigoma Issa Machibya alisema kuwa
kutolewa kwa vifaa hivyo na kutumika katika kituo hicho cya afya ujiji
kutasaidia kupunguza kama siyo kumaliza tatizo la vifo vya  kina mama
wakati wa kujifungua na itakuwa inatimiza lengo la nne la malengo ya
millennia.

Alisema kuwa ni wazi kufungwa kwa vifaa hivyo katika kituo hicho cha afya
kutapunguza msongamano katika hospitali ya Rufaa ya Maweni ambayo ilikuwa
hospitali pekee iliyokuwa ikitegemewa kwa upasuaji na wakazi wa manispaa ya
Kigoma Ujiji.

Baadhi ya kina mama waliohudhuria hafla hiyo wamesema kuwa kufungwa kwa
mashine ya upasuaji kwenye kituo hicho cha afya kutapunguza usumbufu wa
kutegemea hospitali ya maweni ambayo kwao ilikuwa ni hospitali pekee
iliyokuwa ikifanya upasuaji hapa mjini.

Mtendamema Bandora na Hamisa Kassim wakazi wa Ujiji mjini hapa walisema
kuwa kufungwa kwa mashine hizo ni mkom bozi kwao na wametoa wito kwa kina
mama wajawazito kutumia vituo vya afya kwa ajili ya kwenda kujifungulia
badala ya kujifungulia nyumbani au kwa wakunga.

Mwisho.


 

Saturday, November 17, 2012

MAFUNZO YA IJ KIGOMA

Mwandishi wa habari Mkongwe nchini Deodatus Mfugale akisisitiza jambo wakati akiendesha mafunzo ya uandishi wa habari za uchunguzi kwa waandishi wa habari wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoa kigoma KGPC yaliyoendeshwa kwa uwezeshaji wa Muungano wa vilabu vya waandishi wa habari nchini (UTPC) - Picha na Fadhili Abdallah




WAANDISHI wa habari mkoani Kigoma wametakiwa kuandika habari za uchunguzi zitakazozingatia maadili na kuwa na maslahi kwa jamii badala ya kutumia uandishi wa habari za uchunguzi kama nyenzo ya kulipiza kisasi.



Mwandishi wa habari mkongwe nchini, Deodatus mfugale alisema hayo wakati wa mafunzo ya siku sita ya uandishi wa habari za uchunguzi kwa waandishi wa habari wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoa kigoma.


Mfugale alisema kuwa katika kuandika habari za aina hiyo waandishi wa habari wanapaswa kuzingatia hoja zinazoigusa jamii na ambazo haziendi sawa na kwamba uandishi wa habari wa aina hiyo utakuwa na maana kubwa kwa jamii.


Hata hivyo Mfugale alisema kuwa licha ya vyombo vingi vya habari nchini kujisifu kwamba vinaandika habari zilizofanyiwa uchunguzi wa kina bado vingi kati yao havijafikia mahali pa kuandika habari za uchunguzi ambazo zinahitajika kimaadili huku nyingi ya habari hizo zikiacha maswali.


Wakizungumza katika mafunzo hayo waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wanaoshiriki mafunzo hayo wamelalamikia kutokuwepo kwa uwezeshaji kutoka vyombo wanavyofanyia kazi na hivyo kushindwa kufanya kazi ya uandishi wa habari za uchunguzi na kubaki kuandika habari za matukio.


Magreth Magosso mwandishi wa habari wa gazeti la jamb oleo alisema kuwa sambamba na kutokuwepo kwa uwezeshaji vyombo vingi vya habari nchini haviko tayari kuwapatia waandishi wao vitendea kazi na hivyo kufanya kazi ya uandishi wa habari kwa waandishi wa habari hasa wa mikoani kufanya kazi katika mazingira magumu.


Awali Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa kigoma, deo Nsokolo alisema kuwa jumla ya waandishi wa habari 18 wnaatarajia kushiriki mafunzo hayo na kwamba kufanyika kwa mafunzo hayo kutatoa nafasi na kuwapa uzoefu wa utendaji kazi waandishi chipukizi.


Nsokolo alisema kuwa pamoja na mambo mengine mafunzo hayo yanalenga kuwakumbusha waandishi wa habari umuhimu wa kuzingatia maadili, kuwahamasisha kuandika habari za uchunguzi na kuzingatia uzalendo katika kufanya kazi za habari za uchunguzi.


Mwisho.
 

MAFUNZO UANDISHI WA HABARI ZA UCHUNGUZI

 Waandishi wa habari wanachama wa Kigoma Press Club wakifuatilia mafunzo ya uandishi wa habari za Uchunguzi yaliyokuwa yakitolewa na Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari nchini kwa ushirikiano na Kigoma press Club chini ya mkufunzi Nguli Deodatus Mfugale

Mafunzo hayo pia yaluhusisha washiriki kupata chakula mara tatu kwa siku kama ambavyo wanaonekana hapa wakipata chakula lakini wakijikumbusha yaliyojiri darasani

Thursday, November 15, 2012

BALOZI WA KOREA NCHINI JUNG IL ALIPOTEMBELEA DARAJA LA MALAGARASI

 Sehemu ya juu ya kipande cha daraja la Kikwete maarufu kama daraja la Malagarasi ambalo linakaribia kukamilika ambapo Balozi wa Korea nchini Jung IL alitembelea kukagua ujenzi wake kwani daraja hilo linajengwa kwa fedha za mkopo kutoka serikali ya Korea sambamba na kuleta wahandisi kutoka nchini humo
 Balozi wa Korea nchini Jung IL (wa tatu kushoto) na Mkuu wa mkoa kigoma (wa nne kushoto) wakishikana mikono kama ishara ya kupongezana kufuatia mafanikio ya hali ya ujenzi wa daraja la Kikwete (malagarasi) wakati Balozi huyo alipotembelea darajani hapo wa pili kushoto ni Mkuu wa wilaya Uvinza Hadija Nyembo
Mkuu wa mkoa kigoma Issa Machibya (mwenye suti nyeusi) na Balozi wa Korea nchini jung IL (kati kati) wakitembea juu ya daraja la Kikwete (daraja la Malagarasi) kushoto ni Mkuu wa wilaya Uvinza Hadija Nyembo (Picha zote na Fadhili Abdallah)

ZIARA YA BALOZI WA KOREA NCHINI ALIYOIFANYA MKOANI KIGOMA

MKUU WA MKOA KIGOMA ISSA MACHIBYA (KUSHOTO) AKIWA NA BALOZI WA JAMHURI YA KOREA NCHINI KATIKA PICHA

RC AKIKABIDHI MATREKWA KWA WAKULIMA


MKUU wa mkoa Kigoma Issa Machibya (kulia) akizungumza na Viongozi wa halmashauri ya wilaya Kigoma na Manispaa ya Kigoma Ujiji na wakulima wa Tarafa ya nguruka wakati wa Hafla ya kukabidhi matrekta matano kwa wakulima hao

Saturday, October 27, 2012

KIKWETE AWAONYA WANAOVURUGA AMANI

Na Mwandishi Wetu,Kasulu

 Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa serikali haitawavumilia waumin wachache wa madhehebu ya dini wanaotaka kuvuruga amani ya nchi kwa maslahi yao na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kuhusika katika kuchochea vurugu za kidini zinazoendelea nchini. 

Raisi Kikwete alitoa kauli hiyo wilayani Kasulu mkoani Kigoma katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernad Membe wakati wa harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa kanisa katoliki la mtakatifu petro mtume kigango cha Murubona wilayani kasulu.

 kwa upande wake kiongozi wa kanisa hilo , padre Castus Rwegoshora amesema kuwa zaidi ya shilingi milioni mia mbili zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo litakalokuwa na uwezo wa kuchukua waumin elfu mbili kwa wakati mmoja. 


 Katika harambee hiyo zaidi ya shilingi milioni sabini zilipatikana huku huyo wa mambo ya nchi za nje na rafiki zake wakichangia shilingi milioni hamsini.

 mwisho

WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WAKIPEANA MKONO WA EID ELHAJI MKOANI KIGOMA

WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WAKIPENA MKONO KUTAKIANA HERI NA FANAKA YA SIKUKUU YA EID ELHAJI BAADA YA KUMALIZIKA KWA SALA ILIYOFANYIKA KATIKA MSIKITI WA KABONDO UJIJI MKOANI KIGOMA ALIYESIMAMA KATI KATI NI KAIMU SHEIKH WA MKOA HASSA IDDI KIBURWA PICHA NA FADHILI ABDALLAH

Kigoma Press Club: SERIKALI YAELEZA UHABA MKUBWA WA WATAALAM WA AFYA

ASKOFU MKUU WA JIMBO LA TABORA AMBAYE PIA NI MSIMAMIZI WA JIMBO LA KIGOMA LA KANISA KATOLIKI PAUL RUZOKA AKIMUONGOZA NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII DK.SEIF RASHIDI (WA PILI KUSHOTO) NA MKUU WA MKOA KIGOMA ISSA MACHIBYA (WA KWANZA KUSHOTO) KUTEMBELEA MAJENGO YA HOSPITALI YA RUFAA YA KABANGA WILAYANI KASULU MKOANI KIGOMA (PICHA NA FADHILI ABDALLAH)






Na Fadhili Abdallah,Kasulu

SERIKALI imesema kuwa sekta ya afya nchini inakabiliwa na upungufu wa wataalam 62,000 sawa na asilimia 49 ya wataalam wote wanaohitajika na kwamba serikali kupitia kwenye vyuo vyake inatarajia kudahili wastani wa wanafunzi 10,000 kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Waziri Mkuu Mizengo pinda amesema hayo katika hotuba iliyotolewa kwa niaba yake na Naibu Waziri wa afya na ustawi wa jamii, Seif Rashidi wakati akifungua jengo la upasuaji na jengo la wazazi la hospitali ya rufaa ya Misheni Kabanga iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Waziri mkuu alisema kuwa ongezeko hilo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na maboresho akubwa yaliyofanywa kwenye sekta ya afya kwa kupanuliwa kwa hospitali za mikoa na kuzifanya za rufaa na kupanuliwa kwa baadhi ya zahanati kufikia hadhi ya kuwa vituo vya afya.

Alisema kuwa pamoja na mkakati huo wa serikali bado kumekuwa na ongezeko kubwa la hospitali na vituo vya afya vya watu binafsi na mashirika ya dini ambayo serikali inapaswa kusaidia kwa namna yoyote.

Awali Mkurugenzi wa hospitali ya Rufaa ya misheni Kabanga Sebastina Nzebayanga alisema kuwa alisema kuwa hali ya umasikini inayowakabili wananchi wanoishi kuzunguka hospitali hiyo imewafanya kutoza viwango vya chini vya malipo ya huduma inayotolewa hali inayokwamisha kuajiri wataalam wenye sifa hospitalini hapo.

Alisema kuwa kwa sasa hospitali hiyo haina daktari Bingwa wala daktari yeyote mwenye elimu ngazi ya shahada na kwamba hiyo inatokana na kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za mishahara na mahitaji mbalimbali ya wataalam.

Kwa upande wake Meneja miradi wa tume ya kikristo ya huduma za jamii (CSSC), Grace Mwang’onda alisema kuwa kiasi cha shilingi milioni 900 zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo zilizotolewa na serikali ya Ujerumani kupitia benki ya maendeleo ya watu wa Ujerumani.

 Mwang’onda alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya ushirikiano wa serikali za Tanzania na Ujerumani ambapo awamu hii ya pili umehusisha ukarabati wa zahanati 44, uboreshaji wa hospitali nane ikiwemo hiyo ya Kabanga ambayo imepandishwa hadhi na kuwa hospitali ya rufaa.

 Mwisho.