Saturday, October 27, 2012

KIKWETE AWAONYA WANAOVURUGA AMANI

Na Mwandishi Wetu,Kasulu

 Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa serikali haitawavumilia waumin wachache wa madhehebu ya dini wanaotaka kuvuruga amani ya nchi kwa maslahi yao na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kuhusika katika kuchochea vurugu za kidini zinazoendelea nchini. 

Raisi Kikwete alitoa kauli hiyo wilayani Kasulu mkoani Kigoma katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernad Membe wakati wa harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa kanisa katoliki la mtakatifu petro mtume kigango cha Murubona wilayani kasulu.

 kwa upande wake kiongozi wa kanisa hilo , padre Castus Rwegoshora amesema kuwa zaidi ya shilingi milioni mia mbili zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo litakalokuwa na uwezo wa kuchukua waumin elfu mbili kwa wakati mmoja. 


 Katika harambee hiyo zaidi ya shilingi milioni sabini zilipatikana huku huyo wa mambo ya nchi za nje na rafiki zake wakichangia shilingi milioni hamsini.

 mwisho

WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WAKIPEANA MKONO WA EID ELHAJI MKOANI KIGOMA

WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WAKIPENA MKONO KUTAKIANA HERI NA FANAKA YA SIKUKUU YA EID ELHAJI BAADA YA KUMALIZIKA KWA SALA ILIYOFANYIKA KATIKA MSIKITI WA KABONDO UJIJI MKOANI KIGOMA ALIYESIMAMA KATI KATI NI KAIMU SHEIKH WA MKOA HASSA IDDI KIBURWA PICHA NA FADHILI ABDALLAH

Kigoma Press Club: SERIKALI YAELEZA UHABA MKUBWA WA WATAALAM WA AFYA

ASKOFU MKUU WA JIMBO LA TABORA AMBAYE PIA NI MSIMAMIZI WA JIMBO LA KIGOMA LA KANISA KATOLIKI PAUL RUZOKA AKIMUONGOZA NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII DK.SEIF RASHIDI (WA PILI KUSHOTO) NA MKUU WA MKOA KIGOMA ISSA MACHIBYA (WA KWANZA KUSHOTO) KUTEMBELEA MAJENGO YA HOSPITALI YA RUFAA YA KABANGA WILAYANI KASULU MKOANI KIGOMA (PICHA NA FADHILI ABDALLAH)






Na Fadhili Abdallah,Kasulu

SERIKALI imesema kuwa sekta ya afya nchini inakabiliwa na upungufu wa wataalam 62,000 sawa na asilimia 49 ya wataalam wote wanaohitajika na kwamba serikali kupitia kwenye vyuo vyake inatarajia kudahili wastani wa wanafunzi 10,000 kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Waziri Mkuu Mizengo pinda amesema hayo katika hotuba iliyotolewa kwa niaba yake na Naibu Waziri wa afya na ustawi wa jamii, Seif Rashidi wakati akifungua jengo la upasuaji na jengo la wazazi la hospitali ya rufaa ya Misheni Kabanga iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Waziri mkuu alisema kuwa ongezeko hilo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na maboresho akubwa yaliyofanywa kwenye sekta ya afya kwa kupanuliwa kwa hospitali za mikoa na kuzifanya za rufaa na kupanuliwa kwa baadhi ya zahanati kufikia hadhi ya kuwa vituo vya afya.

Alisema kuwa pamoja na mkakati huo wa serikali bado kumekuwa na ongezeko kubwa la hospitali na vituo vya afya vya watu binafsi na mashirika ya dini ambayo serikali inapaswa kusaidia kwa namna yoyote.

Awali Mkurugenzi wa hospitali ya Rufaa ya misheni Kabanga Sebastina Nzebayanga alisema kuwa alisema kuwa hali ya umasikini inayowakabili wananchi wanoishi kuzunguka hospitali hiyo imewafanya kutoza viwango vya chini vya malipo ya huduma inayotolewa hali inayokwamisha kuajiri wataalam wenye sifa hospitalini hapo.

Alisema kuwa kwa sasa hospitali hiyo haina daktari Bingwa wala daktari yeyote mwenye elimu ngazi ya shahada na kwamba hiyo inatokana na kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za mishahara na mahitaji mbalimbali ya wataalam.

Kwa upande wake Meneja miradi wa tume ya kikristo ya huduma za jamii (CSSC), Grace Mwang’onda alisema kuwa kiasi cha shilingi milioni 900 zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo zilizotolewa na serikali ya Ujerumani kupitia benki ya maendeleo ya watu wa Ujerumani.

 Mwang’onda alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya ushirikiano wa serikali za Tanzania na Ujerumani ambapo awamu hii ya pili umehusisha ukarabati wa zahanati 44, uboreshaji wa hospitali nane ikiwemo hiyo ya Kabanga ambayo imepandishwa hadhi na kuwa hospitali ya rufaa.

 Mwisho.
 

MASHEKHE WATAKA WAISLAM WASIUPAKE MATOPE UISLAM

Na Mwandishi wetu,Kigoma Ujiji 

WAUMINI wa dini ya kiislam mkoani Kigoma wameshiriki kwenye ibada ya Eid Alhaji kwa hali ya amani na utulivu ambapo viongozi wa dini na wale wa serikali wameihimiza waislam kudumisha amani na mshimamano miongoni mwa Watanzania. 

Wakizungumza katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo viongozi hao wamesema kuwa amani na usalama ndiyo msingi mkuu wa kuwezesha kufanyika kwa mambo mbalimbali ikiwemo kufanyika kwa ibadi hiyo ya Eid El Haji. 

Akitoa mawaidha kwa waislama waliohudhuria ibada hiyo kwenye viwanja vya msikiti wa Kabondo Ujiji mjini Kigoma Kaimu Shekhe wa mkoa Kigoma, Hassan Iddi Kiburwa amesema kuwa imefika mahali waislama waondoe haya na kuwakemea wale wote wanaotaka kuvuruga amani kwa kisingizio cha dini. 

Akinukuu hadithi za mtume alisema kuwa Mtume aliamrisha watu wa umma wake kuwatendea wema na kuwasamehe wale wanaowakosea badala ya kulipiza kisasi na kuhimiza kuwa waislam kote nchini hawana budi kufuata mafundishi hayo kwani ndiyo msingi wa maisha ya kila siku ya Mwanadamu.

 Alisema kuwa hakuna mahali katika kurani ambako panamfundisha muumini wa dini ya kiislam kupigana au kufanya vitendo vinavyoashiria kuvuruga amani na usalama na kwamba vitendo hivyo vimekuwa vikiupaka matope uislam.

 Naye Mwenyekiti wa jumuia ya kuendeleza Kuran mkoani Kigoma, Hassan Kabeke alisema kuwa vitendo vya uvunifu wa amani na vurugu zinazoendelea nchini zimekuwa na maslahi ya kikundi fulani cha watu ambao wamekuwa wakiwachochea baadhi ya waislam kuungana mkono dhamira yao kwa kutumia dini. 

Alisema kuwa Waisla wanapaswa kulitambua hilo na kuwabaini watu hao ambao kwa namna yoyote hawataki kutii viongozi wao wala kutii mamlaka zilizopo ili kutumiza dhamira zao kwa faida zao binafsi na si kwa maslahi ya dini na waislam kwa ujumla wao. 

Akizungumza kwenye ibada ya Eid El Haji mjini hapa Mkuu wa wilaya kigoma Ramadhani Maneno alisema kuwa vitabu vya dini na hadithi ya mtume Muhamad zinahimiza waislam kupendana na kusameheana pale wanapokuwa wamekwaza na ameeleza kushangazwa na kitendo cha baadhi ya waislam kuhamasisha vurugu na uvunifu wa amani kwa kisingizio cha dini.

 mwisho

SHEKHE GUOGUO

MWENYEKITI WA KAMATI YA MAHUSIANO MEMA YA KIDINI MKOA KIGOMA AMBAYE PIA NI KATIBU WA BARAZA KUU LA WAISLAM (BAKWATA) MKOA KIGOMA SHEIKH SHABAN GUOGUO AKIZUNGUMZA WAKATI WA TAMKO LA VIONGOZI WA DINI KUHUSIANA NA VURUGU ZA KIDINI ZILIZOKUWA ZIKIENDELEA PICHA NA FADHILI ABDALLAH

VIONGOZI WA DINI WAKIIMBA WIMBO WA TAIFA

Viongozi wa madhehbu mbalimbali ya dini mkoani Kigoma wakiimba wimbo wa Tanzania Nakupenda wakati wa mkutano wa viongozi wa dini kutoa tamko kuhusiana na vurugu za kidini zinazoendelea nchini (wanne kushoto) ni Mkuu wa mkoa Kigoma Issa Machibya.

VIONGOZI WA DINI WATOA TAMKO KUHUSU VURUGU

a Fadhili Abdallah,Kigoma 

Viongozi wa madhehebu mbalimbali dini mkoani Kigoma wamekutana na kutoa tamko la pamoja la kulaani vitendo vilivyotokea vya kukojolea kitabu cha Quran, uchomaji makanisa na vurugu zinazoendelea nchini kwa kivuli cha imani ya kidini. 

Viongozi hao wa dini walisema hayo kwenye viwanja vya Mwanga Centre mjini kupitia baraza la mahusiano mema ya kidini katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo mkuu wa mkoa Kigoma Issa Machibya. 

Wa Kwanza kuzungumza katika mkutano huo alikuwa Katibu wa baraza kuu la waislam (BAKWATA) wilaya kigoma, Salum Kabunguru ambaye alisema kuwa baraza hilo linalaani kwa hali yeyote kitendo cha kukojolea kitabu kitukufu cha Quran kilichofanywa huko Mbagala Jijini Dar es Salaam.

 Sambamba na hilo kiongozi huyo wa BAKWATA alisema kuwa baraza hilo pia lina laani kwa nguvu zote uchomaji na uharibifu wa makanisa, kuharibifu makaburi kwa kuvunja misalaba na vurugu nyingine kwa imani ya misingi ya kidini ambayo inavunja amani na utulivu wa nchi. 

 Naye Mchungaji Charles Kitale,Mwenyekiti wa umoja wa makanisa mkoani Kigomaalisema kuwa uvumilifu na ustahimilivu miongoni mwa waumini wa madhehbu mbalimbali ya dini vinahitaji kupewa nafasi kwa kufuata maandiko ya vitabu vya dini zote. 

Alisema kuwa hakuna hata kitabu kimoja miongoni mwa vitabu vya dini ambavyo vinahimiza waumini wake kupigana na kuvuruga amani na utulivu vilivyokuwepo kwani hali hiyo haitoi nafasi kwa ibada za dini hizo kufanyika. .

 Akihitimisha matamko ya viongozi hao wa dini Katibu wa BAKWATA mkoa Kigoma, Moshi Guoguo ambaye ni Mwenyekiti wa baraza la mahusiano mema ya kidini mkoani Kigoma alisema kuwa vurugu za aina yeyote kwa imani za misingi ya kidini hazikubaliki. 

Akizungumza katika mkutano huo Mkuu wa mkoa Kigoma Issa Machibya ametaka viongozi wa dini na waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini kuvumiliana na kuishi kwa upendo na kuonya kuwa serikali haitasita kuwachukulia hatua kali wale wote watakaobainika kuvuruga hali ya amani na utulivu iliyopo mkoani humo. 

Mwisho.

Thursday, June 14, 2012

KAMANDA WA POLISI KIGOMA FRAISSER KASHAI

KAMANDA WA POLISI MKOA KIGOMA FRAISSER KASHAI AKITOA TAARIFA MBALIMBALI KWA WAANDISHI WA HABARI

ADAKWA NA RISASI KIBAO

MAMIA YA RISASI KAMA YANAVYOONEKANA AMBAYO POLISI WALIMDAKA MTU MMOJA ANAYETUHUMIWA KUWA NI JAMBAZI KATIKA MPAKA WA TANZANIA NA BURUNDI

Tuesday, June 12, 2012

JKT KANEMBWA MABINGWA WA SOKA KIGOMA


Na Fadhili Abdallah,Kigoma

TIMU ya soka ya JKT Kanembwa ya wilaya ya kibondo mkoani Kigoma imefanikiwa kunyakua ushindi wa kwanza wa mashindano ya ligi ya taifa ngazi ya Taifa Kituo cha Kigoma baada ya kuibuka na pointi 16 ambazo hazikuweza kufikiwa na timu nyingine sita zilizoshiriki mashindano hayo.

katika mashindano hayo mabingwa hao waliweza kushinda michezo yao mitano na kutoka sare mchezo mmoja na hivyo ushindi huo unaipa tiketi timu hiyo ya Kigoma kucheza ligi daraja la kwanza nchini.

Ushindi wa pili katika kituo hicho cha Kigoma ulichukuliwa na timu ya mwadui ya shinyanga ambayo imeweza kufikisha point 11 baada ya kushinda michezo yake mitatu kutoa sare michezo miwili ambapo ilipoteza mchezo mmoja.


kufuatia kushika nafasi ya pili timu hiyo ya mwadui kutoka shinyanga italazimika kucheza ligi ndogo itakayojumuisha washindi wa pili kutoka vituo vingine ili kupata timu mbili zitakazoungana na timu zilizofuzu kwa ajili ya mshindano ya ligi daraja la kwanza.

Akizungumzia matokeo hayo Kocha wa timu ya JKT Kanembwa Saidi Mdoe amesema kuwa watalazimika kufanya usajili ili kupata wachezaji wa kukiongezea nguvu kikosi chake ili kifanye vizuri kuiwezesha timu hiyo kucheza ligi kuu nchini baada ya miaka 20 ya mkoa Kigoma kupotea katika mashindano hayo.


Kwa upande wake Katibu wa chama cha soka mkoa Kigoma Mrisho Bukuku amesema kuwa  timu hiyo inahitaji kupata wachezaji wenye uwezo wa kuhimili mikiki mikiki ya ligi hiyo daraja la kwanza na kuweza kuipandisha timu hiyo katika ligi kuu nchini.

katika kuunga mkono mafanikio ya timu hiyo Bukuku amesema kuwa uongozi wa serikali wilaya ya kibondo kwa kushirikiana na Mkuu wa mkoa Kigoma, Issa Machibya wamejipanga kutafuta fedha za kuiwezesha timu hiyo kufanya maandalizi ya kutosha na kupata mafanikio katika michezo yake.

mwisho

POLISI YAUA JAMBAZI KIGOMA


Na Fadhili Abdallah,Kigoma

POLISI mkoani Kigoma imempiga risasi na kumuua mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Lowasi Moria anayesadikiwa kuwa jambazi aliyekuwa kwenye mkakati wa kufanya uporaji wa kutumia bunduki kwa mfanyabiashara mmoja wilayani humo.

Kamanda wa Polisi mkoa Kigoma, Fraiser Kashai alisema mjini hapa kwamba kabla ya kutokea mauaji hayo kulitokea kutupiana risasi kati ya polisi na majambazi hayo yaliyokuwa manne na ndipo jambazi mmoja aliuawa na wengine watatu kukimbia.

Kamanda Kashai alisema kuwa baada ya mpambano huo wa kutupiana risasi kati ya polisi na majambazi bunduki moja aina ya SMG iliyokuwa na risasi nne kwenye magazine iliyokuwa ikitumiwa na majambazi hayo imekamatwa.

Akieleza kuhusu tukio hilo Kamanda huyo wa polisi mkoa kigoma alisema kuwa awali polisi ilipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu uwepo wa watu wanne waliokuwa na bunduki ambao walikuwa kwenye mpango wa kumvamia mfanyabiashara mmoja aliyekuwa anasafiri na pikipiki kutoka kakonko kwenda Muhange akiwa na fedha kiasi cha shilingi milioni 12.

Alisema kuwa kufuatia taarifa hizo ;polisi waliweka mtego mahali panapoelezwa kutaka kutokea tukio hilo na ndipo kabla mfanyabiashara huyo hajapita eneo hilo polisi waliwavamia majambazi hayo na kuanza kurushiana risasi zilizopelekea kifo cha jambazi mmoja na wengine watatu kukimbia.


Katika tukio lingine polisi mkoani Kigoma inamshikilia Sara Dasse mkazi wa kijiji cha Mpeta tarafa ya Nguruka mkoani Kigoma kwa tuhuma za kumkaba na kumuua mtoto wake  wa kumzaa aitwaye Zainabu Sitta mwenye umri wa mwaka mmoja.

Kamanda wa polisi mkoani Kigoma, Fraiser Kashai alisema kuwa polisi inaendelea na uchunguzi kuhusiana na mazingira yaliyosababisha kifo hicho lakini alisema kuwa habari za kuaminika zinaeleza kuwa mtuhumiwa anasumbuliwa na maradhi ya akili kwa maana ya ukichaa.

mwisho.

Saturday, June 9, 2012

WAREMBO KABLA YA KUJUA HATIMA YAO WAKAANZA HIVI NA MGONGO KUUMA
WADAU PIA HAWAKUKOSA KILA MMOJA ALIHANGAIKA KIVYAKE KUTAFUTA PICHA NZURI KWA AJILI YA UKUMBUSHO WA TUKIO HILO


Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya Kigoma,Lilian Mbaga ( wa kwanza Kulia) akiwa na warembo wa mkoa Kigoma kwa mwaka huu wa 2012, aliyekaa ni mshindi wa kwanza Anna Willbroad, Mshindi wa pili Suzan Gregory (wa pili kulia) na mshindi wa tatu, Justina Philipo (kushoto)
warembo wa mkoa Kigoma kwa mwaka huu wa 2012, aliyekaa ni mshindi wa kwanza Anna Willbroad, Mshindi wa pili Suzan Gregory (wa pili kulia) na mshindi wa tatu, Justina Philipo (kushoto)

(Picha na Fadhili Abdallah)

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya Kigoma,Lilian Mbaga ( wa kwanza Kulia) akiwa na warembo wa mkoa Kigoma kwa mwaka huu wa 2012, aliyekaa ni mshindi wa kwanza Anna Willbroad, Mshindi wa pili Suzan Gregory (wa pili kulia) na mshindi wa tatu, Justina Philipo (kushoto)

(Picha na Fadhili Abdallah)




Na Fadhili Abdallah,Kigoma

Mwanadada Anna Wilbroad juzi usiku alifanikiwa kunaykua  taji la mnyange wa mkoa Kigoma kwa mwaka 2012 baada ya kuwashinda washiriki wenzake saba walishiriki kinyang'anyiro hicho kwa mwaka huu.


Akitangaza matokeo ya ushindi Jaji mkuu wa mashindano hayo Rashidi Michumino kutoka ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya kigoma Ujiji alisema kuwa pamoja na kunyakua taji hilo mnyange huyo pia atapata zawadi ya fedha taslim kiasi cha shilingi 300,000 na kushiriki katika mashindano ya kanda mkoani Dodoma.

Pamoja na zawadi hizo pia mshindi huyo amepata zawadi ya kusoma kozi ya masomo ua utalii kwa mwaka mmoja katika chuo cha western Tanganyika cha mjini kigoma huku.

Mshindi wa pili katika shindano hilo ulinyakuliwa na mrembo Susan Gregory aliyepata zawadi ya shilingi 200,000 kozi ya masomo ya utalii kwa mwaka mmoja akipata nafasi pia ya kushiriki mashindano ya ngazi ya kanda mkoani Dodoma.

Jaji wa shindano alimtangaza mwanadada Justina Philipo kuwa mshindi wa tatu ambaye alipata zawadi ya fedha taslim kiasi cha shilingi 100,000 kozi ya miezi ya Computer akipata nafasi pia ya kushiriki katika mashindano ngazi ya kanda.

Mwanadada Mwamvita Juma aliibuka kuwa mshindi katika shindano la vipaji na ubunifu ambapo alizawadiwa kiasi cha shilingi 50,000 katika shindano ambalo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya kigoma, Lilian Mbaga alikuwa mgeni rasmi.

Akikabidhi zawadi kwa washindi Mkurugenzi huyo wa Halmashauri ya wilaya kigoma alitoa wito kwa wazazi kuwaruhusu watoto wao kushiriki shindano hilo ambalo kwa sasa limekuwa pia chanzo cha ajira kwa wasichana wanaofanya vizuri na wenye vipaji.

mwisho.

1.PICHA YA JUU NI WAANDISHI WA HABARI WA MKOA KIGOMA WAKIONGOZWA NA MWENYEKITI WAO DEO NSOKOLO KATIKATI WAKITAFAKARI MAMBO KATIKA HOTEL YA LAKE TANGANYIKA MJINI KIGOMA.



2.MKUU WA WILAYA KIGOMA RAMADHANI MANENO AKIFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA MAZINGIRA ULIO CHINI YA MRADI WA MAENDELEO YA BONDE LA ZIWA TANGANYIKA

3.MENEJA WA MRADI WA MAENDFELEO YA BONDE LA ZIWA TANGANYIKA HAWA MSHAMU AKIZUNGUMZA KATIKA MKUTANO WA WATAALAM NA WADAU WA MAZINGIRA KUTOKA WILAYA TATU ZA MKOA KIGOMA NA ZA MKOA KATAVI KUHUSU KUELEZEA HATUA MBALIMBALI ZA UHIFADHI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA YA BONDE LA ZIWA TANGANYIKA (PICHA NA FADHILI ABDALLAH)